Tuesday, 13 September 2016

Jinsi Ya Kuonyesha Heshima.

CHANGAMOTO.

#Mume mmoja anasema “tulipooana, mimi na mke wangu hatukuelewa heshima kwa njia moja. Maoni yetu yalitofautiana. Mara nyingi, nilihisi kwamba mke wangu hanionyeshi heshima anapozungumza nami.” Mke wake anasem “nililelewa katika tamaduni ambazo ni kawaida kuzungumza kwa sauti ya juu, kutumia ishara za uso, na kukatisha wengine wanapozungumza. Mambo hayo hayakuonekana kuwa ni kukosa heshima. Hata hivyo, tamaduni hizo ni kinyume kabisa na zile ambazo mume wangu alizoea.” Heshima ni muhimu sana katika ndoa na haipaswi kupuuzwa hata kidogo. Unawezaje kuonyesha kwamba unamheshimu mwenzi wako wa ndoa?

MAMBO UNAYOHITAJI KUJUA

#Heshima ni uhitaji wa msingi wa wanaume. Kila mtu mmoja-mmoja kati yetu anapaswa kumpenda mke wake kama vile anavyojipenda mwenyewe. Lakini pia kwa upande mwingine, mke anapaswa kumheshimu sana mume wake. Ingawa waume na wake wanahitaji kupendwa na kuheshimiwa, waume wanathamini zaidi kuheshimiwa. Mume anayeitwa David anasema hivi "wanaume wanatamani wake watambue kwamba ni daraka la mume kushughulikia hali, kutatua matatizo, na kuandalia familia.”

#Mke anapomheshimu mume wake kwa kutimiza majukumu hayo, wote wawili hunufaika. Mwanamke aitwaye Doricas anasema,  “Mume wangu hunipenda zaidi ninapoonyesha kwamba ninamheshimu.” Wake pia huhitaji kuheshimiwa.

#Ni kweli kwamba mume humpenda mke wake kwa sababu anamheshimu. Daniel anasema  “Ninahitaji kuheshimu maoni na mapendekezo ya mke wangu. Pia, ninapaswa kujali hisia zake. Ninajua kwamba sipaswi kupuuza hisia zake eti kwa sababu sielewi kwa nini anahisi hivyo.”

#Hivyo heshima inategemea maoni ya mwenzi wako. Wazo si kama unafikiri unamheshimu mwenzi wako, bali yeye anapaswa kuhisi anaheshimiwa. Hilo ni somo ambalo  sisi sote tunajifunza.

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

#Andika sifa tatu za mwenzi wako unazozipenda. Sifa hizo zinaweza kuwa msingi bora wa kusitawisha heshima. Kwa juma moja, chunguza mwenendo wako na si wa mwenzi wako. katika sehemu zifuatazo. Maneno yako. Utafiti mmoja ulionyesha kwamba, “wenzi walio na ndoa imara na zenye furaha hutaja mambo matano mazuri kwa kila jambo moja baya kwa mwenzi wake kila wanapozungumzia matatizo.

#Kwa upande mwingine, wenzi ambao hatimaye hutalikiana, hutaja mambo machache sana mazuri kwa kulinganisha na mabaya. Jiulize hivi: ‘Je, mimi huzungumza na mwenzi wangu kwa heshima? Je, mimi humchambua mara nyingi zaidi ya ninavyompongeza? Mimi hutumia sauti ya aina gani ninapoeleza matatizo au malalamiko yangu?’ Je, mwenzi wako atakubaliana na majibu yako Jaribu kufanya hivi, Jiwekee lengo la kumpongeza mwenzi wako angalau kwa jambo moja kila siku.kufanya hivyo kutachangia amani na furaha ya kweli katika ndoa yenu kwa sababu kutakusaidia kusitawi heshima na uvumilivu kuelekea mwenzi wako.

Pendekezo

#Chunguza tena sifa nzuri kuhusu mwenzi wako. Uwe na zoea la kumwambia mwenzi wako kuhusu sifa zake nzuri ambazo hukuvutia. Mke anayeitwa Alicia anasema hivi “Mimi hutumia muda mwingi sana kufanya kazi za nyumbani, hivyo, mume wangu anapopanga vifaa vyake au kunisaidia kuosha vyombo, mimi huhisi anathamini kazi yangu na kwamba ninatimiza sehemu muhimu katika ndoa yetu.” Jiulize hivi, Je, matendo yangu yanathibitisha kabisa kwamba ninamheshimu mwenzi wangu? Je, mimi hutenga wakati wa kuwa na mwenzi wangu na kumsikiliza kwa makini?’ Unafikiri mwenzi wako atakubaliana na majibu yako? Jaribu kufanya hivi, andika njia tatu ambazo ungependa kuonyeshwa heshima.

#Mwombe mwenzi wako afanye vivyo hivyo. Kisha, mbadilishane orodha hizo ili kila mmoja aboreshe sehemu yake. Jitahidi kutimiza sehemu yako katika kuonyesha heshima. Ukifanya hivyo, mwingine atafanya sehemu yake. Kuna mtu anayesema bila kufikiri kama kwa upanga unaochoma, lakini ulimi wa mwenye hekima huponya. Endeleeni kuvumiliana . . . ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine.

#Upendo hujenga. Brian na Serina wanasema thamani ya mke haitokani tu na majukumu anayotimiza katika familia, kama vile kazi za nyumbani. Anahitaji kujua kwamba sifa zake zinathaminiwa sana. Brian Austin na Carly  pia wanaongezea kwa kusema bila heshima, hamwezi kuwa na ndoa yenye furaha. Badala yake, nyote wawili mtakosa amani na mtakuwa na kinyongo.





No comments: