Saturday, 27 August 2016

Je, Ananifaa?

#Je, Ananifaa? Je, umepata mtu ambaye huenda akafaa kuwa mwenzi wako wa ndoa? Ikiwa ndivyo hivyo, unawezaje kujua ikiwa mtu huyo anakufaa? Ni muhimu kwamba usiangalie mambo kijuujuu. Hii ni kwa sababu yule msichana mrembo zaidi huenda asiwe mwenye kuaminika au yule mvulana maarufu sana huenda asiwe na maadili mazuri.

#Ungependa kumpata mtu ambaye atakustarehesha, mtu ambaye kweli anapatana na utu na miradi yako? Acha kuangalia mambo kijuujuu, mtazame mwenzako bila upendeleo. Hata hivyo, uwe mwangalifu! Huenda ukaona tu mambo unayotaka kuona. Kwa hiyo, usiwe na haraka.

#Jaribu kutambua jinsi rafiki yako alivyo kikweli. Watu wengi wanaoanzisha urafiki wa kimapenzi hawachunguzi mambo kwa undani. Badala yake, wao hutaja tu mambo yanayowapendeza wote wawili, kwa mfano  ‘Tunapenda muziki uleule', ‘Tunapendezwa na mambo yaleyale', ‘Tunakubaliana katika kila jambo!’ Hata hivyo, hupaswi kuchunguza mambo kijuujuu tu.

#Unahitaji kumtambua yule mtu wa siri wa moyoni. Badala ya kukazia fikira mambo mnayokubaliana, huenda mkapata kujuana hata zaidi kwa kuona inavyotokea mnapokosa kukubaliana. Kwa mfano, fikiria mambo yafuatayo, mtu huyu anatenda jinsi gani kutoelewana kunapotokea? Je, anasisitiza maoni yake? Je, ‘analipuka kwa hasira’ na kuanza ‘kutukana’? Au anaonyesha usawaziko, kwa kukubali mambo ili kuwe na amani wakati ambapo hakuna kanuni yoyote inayovunjwa? Je, mtu huyo anapenda kukusukuma ufanye mambo anayotaka, kukutawala, au ni mwenye wivu? Je, anadai umwambie kila kitu unachofanya?

#Fikiria kisa hiki, msichana mmoja anayeitwa Laura anasema hivi: “Mimi husikia kuhusu watu wenye urafiki wa kimapenzi wanaozozana kwa sababu mmoja wao amekasirika kwa kuwa mwenzake hampigii simu na kumweleza mahali alipo. Kwa maoni yangu, hiyo ni dalili ya matatizo." Wengine wana maoni gani kumhusu? Ingefaa kuzungumza na watu ambao wamemfahamu kwa muda fulani, kama vile wazazi au watu wake wa karibu. Kwa njia hiyo utajua ikiwa ‘anashuhudiwa vema.’—Matendo 16:1, 2......#The world is the pity hatuwezi kujua yupi ni rafiki wa kweli mwenye tabia nzuri na asiyefanyizwa na mfumo huu wa mambo.@ Sir Lalian Mwittah Nyalali.

No comments: