Saturday, 27 August 2016

Nafikiria Ngono Saa Zote.

#Unachoweza kufanya,chagua marafiki wako kwa uangalifu. Lakini pia marafiki na wanafunzi wenzako wanapoanza kuzungumza kuhusu ngono, uwe mwenye tahadhari kwasababu kushiriki katika mazungumzo hayo kutafanya iwe vigumu zaidi kwako kudhibiti mawazo yako.Hivyo ondoka mahali penye mazungumzo hayo ili kuepuka kudhihakiwa kulingana na msimamo wako wa kutokuwamo.

#Epuka burudani potovu. Burudani nyingi leo zimekusudiwa kuamsha tamaa zisizofaa za ngono. Biblia inatoa ushauri gani? “Acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.” (2 Wakorintho 7:1)

#Epuka kabisa burudani zinazochochea tamaa za ngono. Je, unaweza kuruhusu virusi vivamie kompyuta yako? Basi kwa nini uruhusu mawazo mapotovu yaingie akilini mwako?

#Kumbuka hili, tamaa za ngono si mbaya. Isitoshe, Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke ili wavutiane, na kutosheleza tamaa ya ngono katika ndoa ni jambo linalofaa. Kwa hiyo, unapopatwa na tamaa kali za ngono, usifikiri kwamba wewe ni mtu mwovu au kwamba huwezi kuishi maisha safi kiadili.

#Jambo kuu, unaweza kuamua kile ambacho utairuhusu akili yako ifikirie. Unaweza kuwa safi katika fikira na mwenendo ikiwa utachagua kufanya hivyo!

Asante sana kwa kutembelea blog hii, na endelea kufanya hivyo ili kupata habari moto moto.

No comments: