Friday, 26 August 2016

MAONI YA VIJANA KUHUSU NGONO.

Kuwafundisha Watoto Kuhusu Ngono ni CHANGAMOTO sana, miaka michache iliyopita, wazazi walikuwa wa kwanza kuwafundisha watoto wao kuhusu ngono. Walifundisha hatua kwa hatua kulingana na umri na mahitaji ya mtoto. Leo mambo yamebadilika. Kitabu THE LOLITA EFFECT kinasema hivi: “Watoto wanapata habari kuhusu ngono wakiwa bado wadogo sana, na habari hizo zimeenea katika vipindi vya burudani za watoto. Je, habari hizo zinawasaidia watoto au zinawaharibu?

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA           KUHUSU NGONO LEO.

#Habari chafu zinapatikana kwa urahisi. Deborah Roffman, katika kitabu chake TALK TO ME FIRST,anasema “mazungumzo, matangazo ya kibiashara, sinema, vitabu, muziki, vipindi vya televisheni, jumbe, michezo, mabango ya matangazo, simu na kompyuta zimejaa picha na lugha chafu za ngono hivi kwamba [watoto na matineja] wanafikiri kwamba ngono ndilo jambo kuu maishani.”

#Wafanyabiashara wamechangia tatizo. Wafanyabiashara hutangaza na kuuza nguo za watoto zinazochochea hamu ya ngono, hivyo tangu wakiwa wachanga, watoto hukazia zaidi mwonekano. Kitabu SO SEXY SO SOON kinasema: “Wafanyabiashara wanajua kwamba watoto hupenda kuiga na kukubaliwa na marika wao, nao hutumia vibaya tamaa hiyo. Lengo kuu la wafanyabiashara ni kuuza bidhaa. Ujuzi pekee hautoshi. Kuna tofauti kati ya kujua jinsi gari linavyofanya kazi na mtu kuwa dereva mzuri, vivyo hivyo kuna tofauti kati ya kujua kuhusu ngono na kufanya maamuzi ya hekima kuhusu ngono.

#Jambo Kuu Leo: Leo, kuliko wakati mwingine wowote, unapaswa kuwafundisha watoto watumie “nguvu zao za ufahamu” ili “kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.” Waebrania 5:14.

#Mambo Unayoweza Kufanya,Wafundishe watoto wako.Ingawa si rahisi kuzungumza na watoto kuhusu ngono, kumbuka kwamba hilo ni daraka lako na unapaswa kulitimiza.Zungumzeni kifupi. Badala ya kutumia muda mrefu kuzungumza na watoto kuhusu ngono, tumia wakati mfupi, kama vile mnaposafiri au kufanya kazi za nyumbani.

#Tumia maswali ya maoni ili kumsaidia mtoto wako kujieleza. Kwa mfano, badala ya kumwuliza, “Je, unapenda matangazo yanayoonyesha picha chafu?” unaweza kumuuliza hivi: “Unafikiri ni kwa nini wafanyabiashara hutumia picha kama hizi ili kuuza bidhaa?” Baada ya kujibu, unaweza kumwuliza: “Unaonaje matangazo hayo?”

#Kanuni ya Biblia: Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.Wafundishe kulingana na umri. Watoto ambao hawajaanza shule wanaweza kufundishwa majina ya viungo vya uzazi na jinsi ya kujilinda na wale wanaotaka kuwatendea vibaya kingono. Kadiri wanavyokua, wanaweza kufundishwa mambo ya msingi kuhusu viungo vya uzazi. Wanapobalehe, wanapaswa kuelewa kwa kina masuala yanayohusu ngono. Wafundishe maadili. Anza kuwafundisha watoto wako umuhimu wa unyofu, heshima na maadili. Kisha, ukiwa umeweka msingi mzuri unaweza kuwafundisha kuhusu ngono.

#Pia, waeleze waziwazi msimamo wako. Kwa mfano, wafundishe kwamba ni vibaya kufanya ngono kabla ya ndoa. Fafanua kwa nini ni vibaya kufanya hivyo. Kitabu BEYOND THE BIG TALK, kinasema: “Vijana wengi hukataa kufanya ngono kwa sababu wanajua kwamba wazazi wao hukataza jambo hilo.”

#Uwe mfano mzuri. Ishi kulingana na maadili unayofundisha. Kwa mfano, je, unachukia mizaha michafu? je, mavazi yako ni yenye kiasi? au unaepuka kuwachezea wengine kingono? Mambo hayo yanaweza kuathiri viwango vya maadili unavyowafundisha watoto wako.

#Uwe na maoni yanayofaa. Ngono ni zawadi kutoka kwa Mungu, na inaweza kuchangia furaha kati ya mume na mke katika ndoa. (Methali 5:18, 19) Mfundishe mtoto wako kwamba baada ya kufunga ndoa atafurahia zawadi hiyo, bila kupata madhara yanayotokana na kufanya ngono kabla ya ndoa.

#1Timotheo 1:18, 19. MAANDIKO MUHIMU “Mlee mvulana kulingana na njia inayomfaa; hata atakapozeeka hatageuka kando na kuiacha.”Methali 22:6. ‘Nawe ukazie [Sheria za Mungu] kwa mwana wako.’Kumbukumbu la Torati 6:6, 7. “Hata hivyo, je, wewe unayemfundisha mtu mwingine, hujifundishi mwenyewe?” Waroma 2:21. Anaandika #Lalian na kusema ili uwe na Uhuru wa usemi na tendo ni lazima uwe wa kwanza kutokushiriki jambo hilo, kiukweli leo si rahsi hata kidogo kwa kijana yeyote kujinasua katika mtego huu, waingeleza wanasema "The Spider Web "..... Traps many youths today.

#DARAKA LA WAZAZI.Licha ya maoni mbalimbali, watoto na matineja huathiriwa zaidi na mwenendo wa wazazi kuliko wa marika wao. Kitabu Talk to Me First kinasema hivi: “Watoto huwategemea sana wazazi kuwaongoza na kuelewa jinsi ya kuishi. Wao hutafuta mashauri kutoka kwa watu wengine wanapojua au kuhisi kwamba wazazi hawataki kuwasaidia.

#Utafiti uliofanywa kwa miaka mingi unaonyesha kwamba watoto ambao hufundishwa na wazazi wao kuhusu ngono hufanya maamuzi mazuri, huwajibika, na zaidi ya yote, huepuka tabia mbaya.”kinasema kitabu *Talk To Me First.

Never ever, dare to keep silent while you know the distinction between two colours. Even if, you are to die because of your stand say "no  once again no.....its like a doctor dealing with  your patient but one has no mathematical precision to tell you about the recovery of your patient in comparison with God, Jehovah......let light gives you an insight of your passage. I, a writer Sir Lalian Mwittah Nyalali.....Thanks for visiting my blog, wish you to keep on, to any updates regard our universe#.

No comments: