1# Fuata Mwongozo wa Mungu ili Uwe na Ndoa Yenye Furaha, yeye aliyewaumba hao kutoka mwanzo aliwafanya mwanamume na mwanamke.”Mathayo 19:4" Yehova, Mungu ndiye aliyeanzisha ndoa ya kwanza. Biblia inasema kwamba alimuumba mwanamke wa kwanza kisha ‘akamleta kwa mwanamume.’ Adamu alifurahi sana hivi kwamba akasema: "Mwishowe huyu ni mfupa wa mifupa yangu na nyama ya nyama yangu". Bado Yehova anataka watu waliofunga ndoa wawe na furaha. Hivyo unapofunga ndoa, huenda ukafikiri mambo yote yatakuwa shwari. Hata hivyo, ukweli ni kwamba hata mume na mke wanaopendana sana watakuwa na matatizo. Katika ufafanuzi huu utapata kanuni mbalimbali zaidi ya hii,ambazo ukizifuata, zitakusaidia kuwa na ndoa na familia yenye furaha.
2#Kubali Jukumu Ulilopewa na Yehova. kwa mujibu wa Biblia mume ndiye kichwa cha familia.Waefeso 5:23. Kama wewe ni mume, Yehova anataka umtunze mke wako kwa upendo. Pia alimuumba akiwa kikamilisho chako, na anataka umthamini na kumpenda. Hivyo ni lazima umpende sana mke wako na uwe tayari kutanguliza mapendezi yake kabla ya mapendezi yako. Vivyo hivyo kama wewe ni mke, mheshimu sana mume wako na kumsaidia kutimiza jukumu lake. Unga mkono kabisa maamuzi yake na ushirikiane naye. Ukifanya hivyo, utamfurahisha mume wako na kumpendeza Yehova.
3#Ni Nini Unachoweza Kufanya? Muulize mwenzi wako jinsi unavyoweza kuwa mume au mke mwema. Sikiliza kwa makini na ujitahidi kabisa kufanya marekebisho, uwe mwenye subira. Japo itachukua muda kwa kila mmoja kujifunza jinsi ya kumfurahisha mwenzake. Lakini kikweli amani ya familia kupitia upendo usio na kifani itasitawi hata zaidi.
4# Pendezwa Kikweli na Hisia za Mwezi Wako.Unapaswa kutanguliza faida za mwenzi wako. Hivyo jitahidi kuonyesha kwamba unamthamini mwenzi wako, na ukumbuke kuwa maneno yanayosemwa bila kufikiri ni kama upanga unaochoma, lakini ulimi wa mwenye hekima huponya. Kwa hiyo, chagua maneno yako kwa busara. Ili kuzungumza kwa fadhili na upendo ndoa yako itadumu hata zaidi.
5#Unachoweza Kufanya, Mwombe Yehova akupe utulivu na usawaziko kabla ya kuzungumzia jambo lolote zito pamoja na mwenzi wako. Fikiria kwa makini mambo utakayosema na jinsi utakavyoyasema.
6#Fanyeni Maamuzi Pamoja. Ni kweli kwamba unapofunga ndoa, wewe na mwenzi wako mnakuwa mwili mmoja.Lakini bado nyinyi ni watu wawili na huenda kila mmoja ana mapendezi yake. Kwa hiyo, mnapaswa kujifunza kuunganisha mawazo na hisia zenu.Umoja ni muhimu mnapofanya maamuzi. Kwa shauri mipango yenyewe hufanywa imara. Fuateni kanuni hii mnapofanya maamuzi hii itaepusha malumbano na mitafaruko isiyo ya lazima ndani ya ndoa. Mbali na kumwambia mwenzi wako habari na maoni yako, mweleze pia hisia zako kwa kuzungumza na mwenzi wako waziwazi kabla ya kufanya makubaliano na mtu mwingine.
7#Kuwa na Usawaziko na Maoni yanayofaa. Usitazamie mengi mno kutoka kwako au kwa mwenzi wako. Kazia fikira sifa nzuri za mwenzi wako. Uwe na hakika kwamba utafaulu ikiwa utafuata kanuni hii ya kuwa na subira. Ukifuata ushauri wake, na ndoa yako itazidi kuimarika mwaka baada ya mwaka.Jiulize hivi,Je mwenzi wangu anahisi kwamba ninamjali kuliko ninavyojijali? Nimefanya nini leo ili kuonyesha kwamba ninampenda na kumheshimu mwenzi wangu?
Hivyo sisi sote tukiwa aidha watoto ama wanandoa tunajukumu la kuchangia usitawi wa furaha na amani ya kweli katika familia.
No comments:
Post a Comment